Mwanaume Amshambulia Mkewe na Panga Kisa Kamnyima Unyumba


KENYA: Mwanamke Ann Akiru(30), anauguza majeraha makubwa mwilini mwake baada ya kushambuliwa kwa panga na mumewe kisa kumnyima unyumba

Mwanaume aliyefanya kitendo hicho, John Lokoreno inadaiwa alijiua baada ya tukio hilo

Akielezea tukio hilo Ann ambaye ni mama wa watoto watano amesema yeye na mumewe wamekuwa na kutokuelewana ndani ya familia yao tangu mwezi Februari

Alimualika mama yake kushuluhisha hali hiyo ya kutokuelewana na kunyima mumewe unyumba na walikubaliana kusonga mbele na kuacha tofauti zao nyuma

Lakini baada ya mama yake kuondoka, mwanaume huyo alirudi nyumbani na kumkuta mke wake akiwa anandaa chakula. Alifunga mlango na kuanza kumshambulia kwa mapanga

Comments